UNAWEZA KUPATA STORI ZETU MOJA KWA MOJA KWA KUBONYEZA 'LIKE' HAPA ➞
« Piga 0652262137 kuweka tangazo lako hapa - Push kwa Buku tu »
Mara kadhaa kwenye familia zetu kikombe cha chupa ya chai kimekuwa kikiorodheshwa kwenye idadi ya vikombe vya plastiki alivyonavyo mtu. Lakini mimi napinga hili.
Kikombe
cha chupa ya chai si kikombe ila ni sehemu ya mfuniko wa chupa ya chai.
Unawezaje kutumia mfuniko na wakati kuna vikombe? Huna tofauti na mtu
anayekunywa soda na kisoda.
Kikombe
cha chupa ya chai ni kwa ajili ya kutoa msaada kwa mfuniko wa chupa ili ikiwa
kuna hali ya baridi toka nje isije ikaingia kupitia mfuniko kirahisi na kile
cha ndani kikapoa. Yaani kikombe kinaongeza usitiri wa kile kilichowejwa ndani
ya chupa kisipoe kirahisi. Kitatumika tu pale ambapo imetokea dharura ya uhaba
wa vikombe kama shambani, safarini, n.k
Sasa
tuachane na hayo maelezo. Ni kitu gani nataka kukuambia muda huu?
Wengi
tunatazama elimu, cheo, nafasi, uwezo, ujuzi, mali, n.k kama ndo njia za
kufanikiwa kwenye maisha. Na tunachukua hivyo vitu kama ndo hatima yetu hapa
duniani na pengine umemaliza yote na sasa “acha roho yako istarehe na kufurahi”.
Kumbuka ya yule tajiri mpumbavu (Lk. 12:13-21).
Mpendwa,
hayo ni ziada tu. Siku ya mwisho hutapimwa kwa elimu, fedha wala chochote
unachokitumainia. Utapimwa kwa sheria ya upendo ambao ni amri kuu. Fedha,
elimu, cheo, nafasi, uwezo, ujuzi, mali, n.k ni nyenzo tu za kujaribu kuonesha
una upendo kiasi gani kwa Mungu na kwa watu wa Mungu, ingawa hata hivyo
haviwezi kukamilisha tafsiri ya upendo pia.
Mungu
anataka utumie hivyo vya nje kiimani ili vitunze kile cha thamani zaidi alichokupa
ndani yako na kwenye maisha yako. Vya nje ni thamani za kidunia, ndani yako kuna
mbegu ya Kimungu ambayo imebeba kusudi la wewe kuumbwa. Basi kuu zaidi ni lile
la ndani ambalo linakuja kuvishwa kilemba na yale ya nje. Hii ina maana kuwa
hata bila ya yale ya nje basi lile la ndani litadumu. Je, kichwa bila kilemba
akili haziwezi kuwepo? Lakini kwenye baridi kilemba chaweza kusitiri kichwa;
hata hivyo akili ya kutafuta kilemba ipo kichwani pia.
Inawezekana
nimeongea kwa ugumu lakini mimi nazungumza kuthaminiana na kuishi kwa upendo wa
kweli kwa Mungu na wanadamu. Usijione bora sana wala kujikweza maana
utashushwa. Kumbuka kilichomuondoa shetani mbinguni ni dhambi ya Kiburi.
Mtu
bora zaidi na anayemtumikia Mungu sawasawa ni yule ambaye maisha yake yameweka
kitu chema kwenye mioyo ya watu kulingana na kile kile alichopewa na uwezo ule
ule aliojaaliwa na Mungu. Ukifa umekufa wewe, lakini hakikisha kuna kitu
kinabaki duniani na kwenye mioyo ya watu ili ijulikane uliishi duniani.
Hakikisha husahauliki kama makapi shambani, tumia kikombe cha chupa ya chai
kutunza joto na si kikombe cha chupa ya chai kunywea chai utapoteza joto la
chupa yako.
Kikombe
cha chupa ya chai ni elimu, cheo, nafasi, uwezo, ujuzi, mali, n.k na joto la
ulichobeba ni lile kusudi la Mungu kwako. Kunywea kikombe cha chupa ya chai ni
kule kutumia ulivyonavyo kuwakandamiza wengine na kuwa na kiburi.
Naitwa Mw. Benson Mmari, Shalom!
Chapisha Maoni
Enenda kwa hekima, ukijua ni yapi yaliyo mapenzi ya Mungu huku ukiukomboa wakati. Install Bewisa App kwenye PlayStore kwa maarifa zaidi.
- EV. BENSON W. MMARI, +255 768 111 279